| Washindi "Kili Time of Your Life"
wapania biashara
Kampuni
ya Bia Tanzania (TBL), kupitia Bia ya Kilimanjaro,
Alhamisi iliyopita ilitangaza washindi wengine tisa
wa droo ya tatu ya shindano la kuburudisha na kutajirisha
la ‘Kili Time Of Your Life’.
Washindi hao wamepatikana kwa njia ya bahati nasibu
na kujinyakulia mamilioni likisimamiwa na Bodi ya
Michezo ya Kubahatisha.
Shindano hili linawawezesha wanywaji
wa Kili kuburudika na kujipatia fedha za kuwasaidia
kuboresha maisha yao.
Mara baada ya Meneja wa Bia ya
Kilimanjaro, Oscar Shelukindo, kuwatangaza washindi
hao, waandishi wa habari walifanya mahojiano na
baadhi yao kwa njia ya simu na kuelezea ndoto zao.
Kwa mfano, Andrea Simon wa Keko
jijini Dar es Salaam anasema kwamba hakuna cha zaidi
anachofikiria, kwani amejipanga kufanya biashara.
“Mimi ni muuza viatu, nina
kaduka kangu (dula langu) hapa Keko, sasa baada
ya kuwasikia wale watu wa Kilimanjaro wakinitangaza
kuwa mshindi nimeona hapa ni mahala pazuri pa kutokea.
Mshindi huyo anasema kwamba alijisikia
vizuri na kujawa na faraja baada ya kushinda, kwani
ameona kuwa huu ni mwanzo wa kujikomboa kiuchumi.
Naye, Elizabeth Raymond wa Mwanza,
ambaye pia amejishindia sh milioni tano, anasema:
“Duh! Eeh, kaka. Hakika nilijsikia raha sana.
Aaah, kaka yangu nina mambo mengi ya kufanya mara
baada ya kupata fedha hizo.
“Kwanza naomba uelewe
kwamba mimi ni mfanyabiashara ambaye nina grocery
(duka la vinywaji) hapa Mwaloni, Mwanza. Halafu
huwa nafuata vitenge Kondo (DRC) hivyo fedha hizo
nitazitumia kutanua biashara zangu,” anasema.
Source:Tanzania Daima
|